Friday, September 5, 2014

IBRAHIMOVIC AVUNJA REKODI YA UPACHIKAJI MABAO


Ibrahimovic amevunja rekodi ya Sven Rydel aliyefunga mabao 49 Sweden


MSHAMBULIAJI wa PSG mabingwa wa soka nchini Ufaransa, Zlatan Ibrahimovic amefanikiwa kuvunja  rekodi ya kuwa mchezaji aliyeifungia mabao mengi zaidi timu ya taifa ya Sweden,baada ya kutupia mabao mawili usiku wa kuamkia leo,ambapo Sweden imechomoza na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Estonia.


Mabao hayo mawili yanamfanya nyota huyo mwenye umri wa miaka 32,kufikisha idadi ya mabao 50,akiipita idadi iliyokuwa inashikiliwa na mchezaji Sven Rydell, ya kufunga mabao 49,na bao lake la mwisho kati ya hayo akilifunga dhidi ya Finland mwaka 1932.


Baada ya kuvunja rekodi hiyo, alitoa jezi yake kuonyesha ujumbe kwa mashabiki uliosomeka. "Ni gjorde det mojligt,' or: wenye maana 'Umefanya iwezekane.'


No comments:

Post a Comment