Saturday, September 6, 2014

STURRIDGE:NIMEVUNJIKA MOYO KUTOITUMIKIA ENGLAND





                                                                          Sturridge
Mshambuliaji Daniel Sturridge,amesema amevunjika moyo baada ya kutupwa nje ya kikosi cha England kitakachocheza mechi yake ya ufunguzi wa patashika ya kufuzu kutinga fainali za Euro 2016 dhidi ya Switzerland keshokutwa jumatatu.

Sturridge, 25,atakuwa nje ya kikosi hicho chini ya kocha Roy Hodgson,baada ya kuumia jana ijumaa wakiwa katika mazoezi na klabu yake ya Liverpool kwenye dimba la St George'Park.

Chama cha soka cha Uingereza FA,kimethibitisha kuwa mchezaji huyo wa Liverpool ataukosa mchezo huo wa kufuzu utakaopigwa mjini Basel.

"kusema kweli nimevunjika sana moyo kuona sitalitumikia taifa langu kwenye mchezo huo,lakini kwa mujibu wa madaktari-nina matumaini ya kurejea uwanjani muda mfupi tu ujao kushirikiana na wenzangu katika mechi zinazofuata,Ni maneno aliyoyaandika Sturridge kwenye mtandao wa kijamii wa Tweeter.

No comments:

Post a Comment