Saturday, September 6, 2014

SINA FURAHA KUONA SIITUMIKII KLABU YANGU

                                               Suarez na mahojiano ya waandishi wa habari


Mshambuliaji mpya wa klabu ya fc Barcelona ya nchini Hispania LUIS SUAREZ amesema amekuwa na wakati mgumu kuitazama timu yake hiyo ikicheza pasipo kutoa msaada wake uwanjani.

SUAREZ hawezi kuitumikia timu hiyo kutokana na adhabu aliyopewa na shirikisho la soka duniani FIFA baada ya kumng’ata meno beki wa timu ya taifa ya italia GIORGIO CHIELLINI katika mashindano ya kombe la dunia 2014 nchini brazil.

Aidha mshambuliaji huyo mwenye miaka 27 aliyetokea Liverpool atakuwa nje ya uwanja mpaka October 25,na amesema itamlazimu kuwa mvumilivu kwa kipindi hiki.

No comments:

Post a Comment