Saturday, September 6, 2014

NITAIDAKIA TIMU YANGU YA CHELSEA KWA MUDA MREFU



Golikipa namba moja wa klabu ya Chelsea na timu ya taifa ya ubelgiji THIBAUT COURTOIS amesema anataraji kusaini mkataba mpya atakaporejea katika klabu yake baada ya mechi za kimataifa kumalizika.

COURTOIS ambaye aliitumikia klabu ya atletico madridi ya nchini Hispania kwa misimu mitatu kwa mkopo amerejea katika klabu yake msimu huu na kuonesha kiwango cha hali ya juu na kumuweka benchi golikipa mkongwe wa klabu hiyo PETER CECH

Aidha kocha JOSE MOURINHO amesema anataraji kumpa mkataba wa miaka mitano Courtois, mwenye umri mdogo baada ya kuonesha kiwango kizuri katika mechi alizocheza.



No comments:

Post a Comment