Saturday, September 6, 2014

KOCHA ENGLAND ATETEA KIKOSI CHAKE

                                        kocha Roy akiwapa maelekezo wachezaji wake


Kocha wa timu ya taifa ya England ROY HODGSON amewatetea wachezaji wa timu hiyo kutokana na mchezo mbovu waliuonesha katika mechi ya kirafiki baina ya timu hiyo na timu ya taifa ya Norway uliopigwa katika uwanja wa wembley na timu hiyo kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila.
HODGSON alichukia baada ya kuulizwa kwanini timu hiyo ilipiga mashuti mawili tu yaliyolenga goli na kujibu kuwa timu hiyo umeundwa na wachezaji wengi wasio na uzoefu hivyo haiwezekani mchezaji alieitumikia timu hiyo kwa mechi 4 mpaka 5 afanye makubwa kama aliyoyafanya DAVID BECKHAM na mchezaji majeruhi kama PHIL JONAS kumfananisha na mkongwe kama JOHN TERRY.
Aidha kocha huyo amesema anajua kuwa idadi ya mashabiki wa taifa hilo inapungua kila siku lakini yeye anachojali nikuhakikiksha timu hiyo inafanya vizuri na atahakikisha wanashinda mechi yao dhidi ya Switzerland jumatatu ijayo.


No comments:

Post a Comment