Saturday, September 6, 2014

RAIS WA REAL MADRID AKANUSHA KUWA NA UGOMVI NA RONALDO

                                  Rais wa Madrid Florentino Perez akiwa na Ronaldo



Rais wa klabu ya Real madridi FLORENTINO PEREZ amesema hakuna hali ya kutoelewana kati yake na mshambuliaji wa klabu hiyo CRISTIANO RONALDO licha ya kuwepo kwa uvumi mbalimbali kuhusu uhusiano wao kwa sasa.

Nyota huyo mapema wiki hii aliponda uamuzi uanaofanywa rais huyo wa kuwauza wachezaji mahiri licha ya kuwa wametoa mchango mkubwa katika kikosi hicho.

 

Aidha PEREZ ambaye anapenda kusajili wachezaji wenye majina makubwa amesema kuuzwa kwa wachezaji kama ANGEL DI MARIA ni uamuzi sahihi kutokana na hela iliyotolewa na klabu ya Manchester united na XABI ALONSO ameuzwa kutokana na yeye mwenyewe kutaka kuondoka.

No comments:

Post a Comment