Friday, August 22, 2014

ARSENAL WAAPA KUMCHUKUA EDINSON CAVAN MSIMU HUU


WABEBA mitutu wa jiji la London Arsenal wanajiandaa kuishawishi klabu ya Paris Saint Germain kwa kuwapa kitita cha pauni milioni 32 pamoja na kumtoa mchezaji Olivier Giroud ili wampate mshambuliaji wao Edinson Cavani.

Cavani amewekwa katika nafasi za juu za wachezaji wanaotakiwa na kocha wa the Gunners, Arsene Wenger,na hii ni baada ya nyota huyo wa Uruguway kuamua kuiacha PSG msimu huu.

Bado haijafahamika kama PSG watakubali ofa hiyo ya Arsenal hasa ikizingatiwa kuwa mshambuliaji wao nyota Zlatan Ibrahimovic amekuwa majeruhi tangu mwishoni mwa wiki.

 


No comments:

Post a Comment