Wednesday, August 27, 2014

EVERTON WANATARAJI MAKUBWA KWA E'TOO

                    Etoo chini ya kocha Morinho enzi hizo wakiwa Inter Milan



Everton inategema kupata huduma nzuri toka kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Cameroon  Samuel Eto'o ,aliyejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili.


Nyota huyo aliyetemwa msimu uliopita na kocha Jose Morinho kwa madai kuwa umri wake umekwenda,ilikuwa asajiliwe na Liverpool lakini dili hilo halikufanikiwa kutokana na klabu hiyo ya Vijogoo kuvutiwa zaidi na mshambuliaji mtukutu Super Mario Balotelli.


Etoo huenda akashuka dimbani kuitumikia klabu yake hiyo mpya katika mchezo wa ligi dhidi ya  Chelsea utakaopigwa siku ya Jumamosi. 


Mshambulizi huyo ambaye aliwahi kuwa mchezaji nyota barani Afrika kwa miaka minne aliifungia Anzhi Makhachkala mabao 12 katika mechi 35 alizoshiriki.


Amewahi kuvitumikia pia vilabu vya ligi kuu ya Hispania Real Madrid na Barcelona,na wakati akiwa huko  Nou Camp, alitwaa ubingwa wa ligi ya Ulaya mara mbili katika mwaka wa 2006 na 2009 .


Itakumbukwa kwamba Eto'o alijiunga na Inter Milan 2009 kutokea Barcelona alipoisaidia kutwaa kombe la mabingwa chini ya Mourinho huko San Siro.


Everton tayari wamemsajili Romelu Lukaku kutoka Chelsea kwa gharama ya pauni milioni £28,pamoja na  Christian Atsu wa mkopo.

No comments:

Post a Comment