Sunday, August 31, 2014

IVORY COAST YAITUNISHIA KIFUA CAF-MECHI YAKE DHIDI YA SIERRA LEONE (AFCON)

                                                         Majembe ya Tembo wa Ivory Coast

Shirikisho la soka la IVORY COAST,lipo njia panda kuamua kama watacheza mechi yao ya kufuzu kwa fainali za mataifa ya afrika dhidi ya wapinzani wao SIERRA LEONE au la,kutokana na hofu ya ugonjwa wa Ebola.


Mechi hiyo muhimu kwa pande zote mbili,imepangwa kuchezwa jumamosi ya septemba 6 mwaka huu,huko mjini Abidjan,lakini taarifa toka serikali ya Ivory Coast inasema maafisa wa afya wan chi hiyo,wanaweza wakati wowote kutangaza kuipiga marufuku mechi hiyo,kutokana na ukweli kwamba mataifa 5 ya kanda ya Afrika Magharibi yamekumbwa na ugonjwa huo wa Ebola ikiwemo Sierra leone yenyewe.


SIERRA LEONE imeagiza maafisa wote wa ukufunzi kufanyiwa uchunguzi wa kutosha kabla ya kuingia IVORY COAST na Tayari SIERRA LEONE imetaja kikosi cha wachezaji wanaocheza nje ya Sierra Leone ilikuepusha hatari ya kueneza Ebola IVORY COAST. 


Kwa upande wake Shirikisho la soka barani Afrika CAF limekataa kufanya mabadiliko yeyote ya mechi hiyo,na kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo huenda Ivory Coast ikachukuliwa hatua ingawa haijulikani kama CAF watafanya hivyo.


No comments:

Post a Comment