Sunday, August 31, 2014

RONALDO AMPONDA TENA MESSI TUZO YA MCHEZAJI BORA KOMBE LA DUNIA

                                                               Ronaldo akipokea tuzo
           Messi akipokea tuzo ya mchezaji bora wa dunia-204 kwa mshangao

Siku chache baada ya Mshambuliaji nyota wa klabu ya REAL MADRID na timu ya taifa ya Ureno CRISTIANO RONALDO,kupokea tuzo ya kuwa mchezaji bora barani ulaya,nyota huyo amemkejeli nyota nyota mwenzake wa klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya Argentina LIONEL MESSI, kwa kusema kuwa mshambuliaji huyo hakustahili kupewa tuzo ya mchezaji bora wa mashindano ya kombe la dunia ya mwaka huu yaliyomalizika huko nchini Brazil.

RONALDO alinukuliwa akisema,’nikisema kila kitu naweza kuchukuliwa hatua na kupelekwa gerezani,lakini ukweli ni kwamba Messi hakustahili kupewa tuzo’alisema Ronaldo.

 Wadadisi wa mambo wamesema kauli hiyo inaweza kuamsha uhasama wa maneno kati ya wachezaji hao wawili walio bora duniani,licha ya wao wenyewe kusema kuwa hawana ugomvi wowote.

Messi hakuonesha uwezo mkubwa katika mashindano hayo ya dunia,sambamba na Ronaldo mwenyewe,lakini akajikuta akikabidhiwa tuzo hiyo iliyomfanya hata yeye mwenyewe kuishangaa.

Mchawi huyo mweupe wa soka duniani, alipewa tuzo hiyo baada ya kuwapiku wapinzani wake THOMAS MULLER na mfungaji bora wa mashindano hayo JAMES RODRIGUEZ,baada ya kufanikiwa kuweka nyavuni mabao 4.

No comments:

Post a Comment