Sunday, August 31, 2014

KOCHA LIVERPOOL AMUONYA BALOTELLI NA VITUKO VYAKE

                              Balotelli akiwa na kocha wake mpya Brendan Rodgers


Kocha wa Liverpool Brenden Rodgers, amemuonya mshambuliaji wake mpya kutoka AC Milan mtukutu Super Mario Balotelli,kwamba klabu haitokuwa tayari kumfiria yeye tu hivyo anatakiwa kufuata taratibu na sheria toka kwa viongozi wake.

Kocha Rodgers, amesema anajua kuwa Balotelli ni mchezaji mkubwa na mwenye kipaji na anatakiwa kudhihirisha ubora wake kwa kuonesha kandanda zuri pamoja na ushirikiano kwa viongozi pamoja na wachezaji wenzake aliowakuta.

Liverpool imemsajli Balotelli hivi karibuni ili kuziba pengo lililoachwa na mshambuliaji Luis Suarez,aliyejiunga na klabu ya Barcelona ya Hispania.

Tayari nyota huyo ameshaanza kuwa gumzo katika maeneo mbalimbali huko Uingereza kutokana na vituko vyake ndani na nje ya uwanja.

No comments:

Post a Comment