Monday, September 1, 2014

KLUVERT AITAKA KLABU YA SCOTLAND

                                                     Kluvert (kulia) akiwa na Van Gaal (kushoto)


Baada ya kukosa nafasi ya kuwa kocha msaidizi katika klabu ya Manchester united, mchezaji wa zamani wa klabu ya FC Barcelona na timu ya taifa ya Uholanzi, Patrick Kluvert,sasa ameelekeza nguvu zake kuomba nafasi ya kuwa kocha mkuu wa klabu ya Ross County ya nchini Scotland.

Mwenyekiti wa klabu hiyo Roy MacGregor amethibitisha kuwa Kluvert ni miongoni mwa makocha walioleta maombi ya kutaka kuinoa klabu hiyo,lakini atakutana na upinzani mkali kutoka kwa kocha wa zamani wa klabu ya St Mirren ambaye naye anahitaji nafasi hiyo.

Kluvert ,alikuwa kocha msaidizi katika timu ya taifa ya uholanzi katika mashindano ya kombe la dunia nchini brazil chini ya kocha Luis Van Gaal anayeinoa Manchester united.


No comments:

Post a Comment