Monday, September 1, 2014

GUARDIOLA ANAFAA KUIONGOZA TIMU YA TAIFA ARGENTINA:MENOTTI

                                       Kocha Guardiola akishangiliwa baada ya ubingwa


Kocha aliyeipa ubingwa wa kombe la dunia timu ya taifa ya Argentina mwaka 1978, Luis Menotti, amesema kocha wa zamani wa klabu ya Barcelona ambaye kwa sasa anakinoa kikosi cha Bayern Munich Pep Guardiola ,atakuwa kocha wa Argentina kama taifa hilo litaonesha nia ya kumuhitaji.


Menotti, amesema alizungumza na kocha huyo raia wa Hispania na akamwambia kuwa anatamani kuwa kocha wa taifa hilo ingawa anahisi viongozi wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Argentina hawatapenda aina ya ufundishaji wa Guardiola.


Argentina haijapata kushangilia ubingwa wa kombe la kopa  Amerika tangu mwaka 1993 na Menotti anaamini kuwa timu hiyo itanyakua ubingwa huo mwakani ikiwa chini ya kocha Guardiola.

No comments:

Post a Comment