Shirikisho la soka la
IVORY COAST,kwa idhini ya serikali ya nchi hiyo,imekubali kucheza mechi yake ya
kufuzu kwa fainali za mataifa ya afrika dhidi ya wapinzani wao SIERRA LEONE.
Awali Ivory Coast
ilitishia kukataa kucheza mechi hiyo kutokana na tishio la ugonjwa wa
Ebola,baada ya kuzingatia kwamba nchi za afrika magharibi zilizoripotiwa
kukumbwa na ugonjwa huo mbaya,Siera Leone nayo imo.
Hata hivyo licha ya
kuwemo kwa tishio hilo la Ebola,shirikishoa la soka barani afrika
CAF,lilishikilia msimamo wake kwamba mechi hiyo ni lazima ipigwe huko Abidjan
nchini Ivory Coast kama ilivyopangwa.
Mechi hiyo muhimu kwa
pande zote mbili,imepangwa kuchezwa jumamosi ya septemba 6 mwaka huu,lakini
hapo kabla SIERRA LEONE iliagiza maafisa wote wa ukufunzi kufanyiwa uchunguzi
wa kutosha kabla ya kuingia IVORY COAST.

No comments:
Post a Comment