Thursday, August 21, 2014

NADAL: SITASHIRIKI MASHINDANO YA US OPEN

RAFAEL NADAL


Matumaini ya Bingwa namba mbili wa mchezo wa Tenis duniani,Rafael Nadal,kupona haraka jeraha la kifundo cha mkono wake yameyeyuka baada ya adaktari wake kusema kwamba itamchukua muda wa siku kadhaa kupona jeraha hilo.

Nadal alilazimika kujiondoa katika mashindano ya US Open kutokana na jeraha hilo  la kifundo cha mkono wa kulia,na hivyo kuwafanya mashabiki wake kukosa uhondo walioutegemea toka kwa manatenesi wao mashuhuri.

Nyota huyo alipata jeraha alipokua kwenye mazoezi mwezi julai hali iliyomfanya kushindwa kuhudhuria mechi mbili za kujipima nguvu.

No comments:

Post a Comment