Suarez akiwa mazoezini na wenzake
Kocha wa Barcelona,Luis Enrique,amesema
kuwa mshambuliaji wake mpya aliyemnunua toka Liverpool- Luis Suarez ,atashuka
dimbani leo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa kandanda nchini
Mexico-Club Leon.
Suarez aliyekuwa akijifua vilivyo
ili kubaki katika kiwango chake kilichowavutia Barcelona kiasi cha kumnunua kwa
kiasi kikubwa cha pesa,atashuka dimbani hii leo lakini kwa mujibu wa kocha
wake,hatoweza kumaliza dakika zote 90.
Nyota huyo raia wa Uruguway,hivi karibuni amekumbana na adhabu ya kutojihusisha na kandanda baada ya kumng'ata meno mchezaji wa timu ya taifa ya Italia,katika patashika ya kombe la dunia huko Brazil.
Nyota huyo raia wa Uruguway,hivi karibuni amekumbana na adhabu ya kutojihusisha na kandanda baada ya kumng'ata meno mchezaji wa timu ya taifa ya Italia,katika patashika ya kombe la dunia huko Brazil.
Itakumbukwa pia mwaka uliopita
Suarez alilazimika kuomba radhi kutokana na kitendo chake cha kumng’ata meno
beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic na
kukumbana na adhabu ya kutocheza mechi 10.
|
Desemba mwaka 2011,alifungiwa
kutocheza mechi 8 na kupigwa faini ya pauni elfu 40 kwa kuonesha ubaguzi
dhidi ya mchezaji wa Manchester
United, Patrice Evra, na mwezi novemba mwaka 2010,alifungiwa kutocheza mechi
7 kwa kumng’ata bega mchezaji wa PSV Endhoven-Otman Bakkal wakati akiichezea
klabu ya Ajax.
|


No comments:
Post a Comment