Sunday, August 17, 2014

STURRIDGE:LIVERPOOL BILA SUAREZ INAWEZEKANA


                                                                 Raheem Sterling

Mshambuliaji Daniel Sturridge,amefunguka na kusema kuwa klabu yake ya Liverpool ipo imara msimu huu hata bila ya kuwepo mshambuliaji nyota mtukutu Luis Suarez,muda mchache tu baada ya kuisambaratisha mabao 2-1 klabu ya Southampton katika mchezo uliopigwa usiku wa kuamkia leo.


Katika mchezo huo Liverpool walitawala kipindi chote cha kwanza na kufanikiwa kupata bao katika dakika 23 likifungwa na Raheem Sterling  kabla ya mchezaji Clyne kuisawazishia klabu yake katika dakika 56,na baadaye Daniel Sturridge katika dakika ya 79 akapigilia msumari wa mwisho kwa kuandika bao la pili na la ushindi.


Sturridge ametoa kauli hiyo alipoulizwa kama Liverpool itakuwa bora msimu huu licha ya kumuuza Suarez,na kusisitiza kuwa kutokana na wachezaji waliowanunua msimu huu,hakuna ubishi kwamba kikosi hicho sasa ni moto wa kuotea mbali.


Liverpool mpaka sasa msimu huu,imewasajili beki  Javier Manquillo, 20,kwa mkopo akitokea kunako klabu ya Atletico Madrid,mshambuliaji Divock Origi, 19, aliyetokea klabu ya Lille ya Ufaransa pamoja na mlinzi Alberto Moreno, 22,aliyesajiliwa kutoka klabu ya Sevilla.


Wengine ni, Rickie Lambert, 32,na Adam Lalana,25 waaliyesajiliwa kutoka klabu ya Southampton, kiungo Emre Can, 20, toka Bayer Leverkusen ya Ujerumani,Wingea Lazar Markovic, 20, toka klabu ya Benfica ya Ureno pamoja na mlinzi Dejan Lovren, 25,toka klabu ya Southampton.

Usajili wa wachezaji wote hao umeigharimu Liverpool kitita cha pauni milioni 101.


No comments:

Post a Comment