Sunday, August 17, 2014

MANCHESTER CITY IPO TAYARI KUUTETEA UBINGWA WAKE

Aguero
                                                                          Silva

Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya England Manchester City,wameanza vema utetezi wao baada ya kuionesha kandanda la uhakika klabu ya Newcastle United waliokuwa nyumbani kwao,kwa kuitandika mabao 2-0 na kujikusanyia pointi zote tatu muhimu.


Bao la kwanza limepatikana katika kipindi cha kwanza likifungwa na mchezaji David Silva katika dakika ya 39 baada ya kupokea pasi murua toka kwa Eden Dzeko,kabla ya mshambuliaji Sergio Aguero katika dakika ya 90 hajakwamisha mpira wavuni na kuandika bao la pili.


Ushindi huo unaonesha matumaini kwa City kufanya vizuri katika msimu huu na kulitetea tena taji lake,licha ya kushindwa kunyakua taji la ngao ya hisani mbele ya Arsenal katika mchezo wa ufunguzi wa ligi.


Kocha Manuelle Pellegrini,amesema hana wasiwasi hata kidogo na kikosi chake alichokisuka vema,na ana uhakika kuwa safu zake zote zipo tayari kwa mapambano ya ligi.

                                                                                                                                

No comments:

Post a Comment