Thursday, August 28, 2014

PEP GUARDIOLA : MEHDI BENATIA ATATUSAIDIA SANA

                                                              Benatia akiwa katika moja ya hekaheka

Beki mpya wa klabu ya Bayern munich na timu ya taifa ya morocco MEHNDI BENATIA amesema kuitumikia klabu hiyo ni ndoto yake ya muda mlefu na amefurahi kupata nafasi ya kuwa chini ya Kocha PEP GUARDIOLA katika hiyo.
 
Mabingwa hao wa ligi ya bundesliga walithibitisha  kuwa wamefikia makubaliano na klabu ya AS ROMA ya nchini itali ya kumchukua mchezaji huyo mwenye miaka 27 ,ambaye amesaini  mkataba wa muda mrefu wa  miaka mitano.


BENATIA aliekuwa beki muhimu katika klabu ya AS ROMA tangu ajiunge na klabu hiyo akitokea klabu ya Udinese msimu uliopita, amekuja kuziba nafasi ya JAVI MARTINEZ ambaye atakua nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na kuumia kifundo cha mguu.

No comments:

Post a Comment