Thursday, August 28, 2014

MCHEZAJI MKONGWE AS ROMA ATAMBA BADO YUKO FITI

                                                                          FRASCESCO TOTTI (10)



Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya italia anaekipiga kunako klabu ya AS Roma FRANCESCO TOTTI amesema hafikirii kustaafu soka kwa sasa ingawa hana furaha na mchezo kama ilivyokuwa zamani kutokana na wachezaji wa kisasa kitumia nguvu nyingi.

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 37 aliyeitumikia AS ROMA tangu mwaka 1993 na ameichezea klabu hiyo zaidi ya mechi 650, amesema nikweli anaelekea kwenye utu uzima lakini bado ana kiwango kizuri kuliko wachezaji wenye umri mdogo.

Aidha mkongwe huyo aliyeifungia ROMA magoli 26 msimu uliopita amesema mambo yamebadilika kunako klabu hiyo na anaandika kitabu kuhusu marais, makocha na wachezaji wote walioingia na kutoka katika klabu hiyo tangu ajiunge nayo mwaka 1993.

No comments:

Post a Comment