Kocha wa Manchester United LOUIS VAN GAAL amewaudhi wapenzi wa
klabu hiyo baada ya kusema kuwa hakushangazwa na kichapo cha mabao 4-0 mikononi
mwa klabu dhaifu ya MK DONS iliyo katika nafasi ya saba katika msimamo wa
ligi daraja la kwanza katika mechi ya kuwania ubingwa wa kombe la
Capital One .
Kocha huyo alisema kuwa timu haijengwi kwa mwezi mmoja hivyo
anahitaji muda kidogo akiwa kama kocha wa timu hiyo ili kuweka mambo sawa na Kufuatia kipigo hicho kocha huyo raia wa uholanzi ameongeza
nguvu zake kwa kiungo wa klabu ya juventus ARTURO VIDAL kwa kutoa ofa ya paundi
milioni 33.4 ili kupata huduma ya mchezaji huyo kutoka nchini chile.
United tayari
wametumia zaidi ya paundi milioni 132 katika usajili baada ya kutoa paundi
milioni 59.7 kumnunua ANGEL DI MARIA kutoka Real Madrid na bado wanataka
kuongeza wachezaji kabla dirisha la usajiri kufungwa siku ya jumatatu ili
kuepusha maandamano yaliyopangwa kufanywa na mashabiki wa klabu hiyo kutokana
na mwenendo mbovu wa klabu yao..


No comments:
Post a Comment