Friday, August 22, 2014

REAL MADRID YAKOSA NDOO YA SUPER CUP NA RONALDO AKIWEMO

                                       Mario Mandzukic akishangilia bao alilofunga


KIKOSI cha Real Madrid kimeshikishwa adabu na wapinzani wao Atletico Madrid kwa kuchapwa bao 1-0 katika mchezo wa fainali ya michuano ya kuwania Super Cup,mchezo uliopigwa usiku wa ijumaa.

Itakumbukwa kuwa katika mchezo wa kwanza uliopigwa kunako dimba la Camp Nou,timu hizo zilikwenda sare ya kufungana bao 1-1,na matokeo hayo yanaifanya Atletico kuchomoza na ushindi wa jumla wa mabao 2-1.

Mfungaji aliyepeleka kilio kwa Madrid ni Mario Mandzukic,aliyejiunga na  Atletico akitokea Bayern Munich,bao ambalo amelifunga katika dakika ya pili tu ya mchezo.

No comments:

Post a Comment