Monday, August 25, 2014

UONGOZI YANGA WAPEPESA MACHO HATIMA YA MTUKUTU OKWI

                                     Waganda Hamis Kiiza na mtukutu Emanuel Okwi


Uongozi wa klabu ya Dar Young Africans bado unaendelea kupepesa macho na kung'ata maneno kuhusu hatima ya mshambuliaji wao mganda Emanuel Okwi,ambaye amekuwa akiwasumbua tangu alipojiunga na klabu hiyo ya jangwani.


Taarifa toka kwa katibu mkuu wa yanga Beno Njovu,imesema nyota huyo aliyerejea hivi karibuni toka nyumbani kwao Uganda hatokwenda kujiunga na wenzake walioweka kambi huko Zanzibar na badala yake ataendelea kubaki jijini mpaka wenzake watakaporejea.


Mpaka sasa uongozi wa yanga haujatoa uamuzi ni mshambuliaji gani watakayemfungashia virago kati ya Emanuel Okwi na Hamis Kiiza wote toka nchini Uganda,wakidai kuwa jukumu la kusema ninani abaki kwenye kikosi hicho lipo mikononi kwa kocha wao mpya M-brazil Maxio Maximo.


Okwi alisajiliwa na yanga kwa ushawishi wa Hamis Kiiza ambaye alifikisha asilimia 98 za kutimuliwa kwake huku klabu hiyo ikiwa haijui ni vipi watampata Okwi,na baadaye Kiiza kudai kuwa yeye anauwezo wa kumshawishi mganda mwenzie kuja kujiunga na yanga, lakini kwa mashariti kwamba mpaka naye apewe mkataba ndipo afanye kazi hiyo.


Baada ya Okwi kuwasili na kiiza kupewa mkataba,uongozi wa jangwani chini ya mwenyekiti wake Yusuph Manji,kwa sasa unaonesha wazi kuwa hautaki kubaki na wachezaji wote kwa pamoja na badala yake wanataka kutema mmoja wao,na kwa mujibu wa taarifa ilizoifikia blog hii ni kwamba kiiza yupo karibu zaidi na mlango wa kutokea.

Yanga ipo kambini huko Zanzibar kwaajili ya maandalizi ya michuano ya ligi kuu,na watashuka dimbani kukipiga dhidi ya Mabingwa Azam FC kuwania ngao ya jamii.






No comments:

Post a Comment