Friday, September 5, 2014

WAVUMILIENI COTINHO NA JAJA WAONESHE VITU VYA KIBRAZIL:MAXIMO


Yanga wakiwa Mazoezini pamoja na Cotinho,Jaja

KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Mbrazil Marcio Maximo amewaambia wanachama na wapenzi wa timu hiyo, wawavutie subira wachezaji wapya waliosajiliwa ili wazoee na kuanza kufanya vitu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo, makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam, Maximo amesema wachezaji Wabrazil wenzake, kiungo Andrey Coutinho na mshambuliaji Geilson Santana Santos ‘Jaja’ wote ni wazuri.

“Hawa wachezaji wapya wa Brazil wote ni wazuri, Coutinho na Jaja wataisaidia timu, mashabiki na wapenzi wawape muda, waache kuwazomea,”amesema Maximo.

Maximo alikuwa akizungumzia mchezo wa kirafiki wa Jumapili dhidi ya Bata Bullets ya Malawi, ambao amesema utakuwa wa mwisho kabla ya kumenyana na Azam FC katika mechi ya Ngao ya Jamii Septemba 14.

Amesema baada ya mechi hiyo, timu yake itaingia kambini kujiandaa na mchezo wa Ngao dhidi ya Azam FC, ambao ni mabingwa wa Tanzania Bara.

Tayari Yanga SC imekwishacheza mechi nne za kujipima chini ya Maximo tangu aanze kazi Julai na kushinda zote, 1-0 mara mbili dhidi ya Chipukizi ya Pemba na Thika United ya Kenya na 2-0 pia mara mbili dhidi ya Shangani na KMKM zote za Zanzibar. Coutinho na Jaja wote wamefunga mabao mawili kila mmoja katika mechi hizo nne.

No comments:

Post a Comment