Thursday, September 4, 2014

ANGEL DI MARIA AIANGAMIZA UJERUMANI JANA USIKU

                                                                                      Angel Di Maria

Mchezaji mpya wa Manchester United aliyesajiliwa kwa dau la kuvunja rekodi msimu huu, Angel Di Maria,ameonesha kile atakachoifanyia klabu yake hiyo mpya,baada ya jana usiku kutengeneza nafasi tatu zilizozaa magoli na mwenyewe kutumbukiza la kwake,wakati Argentina ikilipa kisasi kwa Ujerumani kwa kuitandika mabao 4-2.

Di Maria,aliyesajiliwa kwa kitita cha pauni milinoni 59.7,alianza makeke yake kwa kutengeneza pasi kwa Sergio Aguero,aliyekwenda kufunga bao la kwanza katika dakika ya 20,kabla ya kumtengenezea pasi nyingine Erik Lamela,aliyefunga bao la pili katika daika ya 40.

Hali hiyo ikazidi kumchanganya kocha wa Ujerumani Joachim Low,ambaye aliingia uwanjani kutaka kuendeleza ubabe kwa Argentina baada ya mwezi julai kuifunga bao 1-0 katika fainali ya kombe la dunia huko Brazil,lakini mambo hayakuwa kama alivyofikiria.

Katika dakika ya 48 Di Maria akafanya kazi nzuri nyingine kwa kumpa pasi yenye manufaa Fernandez,aliyefunga bao la tatu,na alipoona amechoka kutoa pasi kwa wenzake akaamua kutumbukiza mwenye bao la 4 katika dakika ya 50,kabla ya mchezaji wa Chelsea Andre Schurrle na Mario Gotze kuipatia Ujerumani mabao 2 katika dakika ya 52 na 78.
………………………………………………………………………………
VIKOSI KAMILI KATIKA MCHEZO HUO

Germany

  • 01 Neuer (Weidenfeller - 45' )
  • 15 Durm
  • 02 Großkreutz
  • 03 Ginter
  • 04 Höwedes (Rüdiger - 77' )
  • 21 Reus
  • 18 Kroos (Rudy - 71' )
  • 24 Kramer
  • 09 Schürrle (Müller - 57' )
  • 14 Draxler Booked (Podolski - 33' Booked )
  • 23 Gomez (Götze - 58' )

Substitutes

  • 05 Hummels
  • 07 Rudy
  • 10 Podolski
  • 12 Zieler
  • 13 Müller
  • 19 Götze
  • 20 Boateng
  • 22 Weidenfeller

Argentina

  • 01 Romero (Andujar - 80' )
  • 04 Zabaleta (Campagnaro - 77' )
  • 16 Rojo
  • 15 Demichelis Booked
  • 17 Fernández
  • 06 Biglia
  • 14 Mascherano
  • 08 Pérez (Fernández - 45' )
  • 10 Agüero (Gaitán - 83' )
  • 18 Lamela (Gago - 68' )
  • 07 Di María (Álvarez - 86' )

Substitutes

  • 03 Campagnaro
  • 05 Gago
  • 09 Higuaín
  • 13 Fernández
  • 19 Álvarez
  • 20 Gaitán
  • 21 Andujar
  • 22 Lavezzi
  • 23 Basanta



No comments:

Post a Comment