Thursday, August 14, 2014

AGUERO AWAFUATA KINA KOMPANY,SILVA-KUFIA MAN CITY.

                                                           Sergio Aguero

Mshambuliaji wa mabingwa wa kandanda wa England Manchester City, Sergio Kun Aguero,amekubali kuongeza muda wa mkataba wake na sasa utamfanya aitumikie klabu hiyo hadi mwaka 2019,baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano. 


Aguero,27-anaungana sasa na wenzake David Silva na Vicent Kompany kusaini kandarasi ndefu ya miaka mitano,lakini anaungana pia na wachezajji wengine kama, Samir Nasri na Aleksandar Kolarov,ambao nao wameongeza mikataba yao kusalia Etihad Stadium. 

Itakumbukwa Aguero,ameweka historia ya kufunga bao la dakika ya mwisho ambapo City imefanikiwa kutwaa taji la ligi kuu ya England,siku ya mwisho ya kufunga msimu wa mwaka 2011/2012.

Amefanikiwa kufunga jumla ya mabao 75  katika mechi 122 akiwa na klabu yake hiyo ya Manchester City.

No comments:

Post a Comment