Tuesday, August 12, 2014

DAVID SILVA AAPA KUFIA MANCHESTER CITY

Kocha Manuelle Pelegrini akiwa na David Silva
 vijana wa Man City wakisherehekea ubingwa wa England

Kiungo mshambuliaji David Josue Jimenez Silva,ana ndoto za kunyakua taji la mabingwa ulaya,na ameiweka mbele Manchester City kwamba ni moja kati ya vilabu vitakavyofanya hivyo na ndio maana ameamua kuongeza mkataba wa miaka mitano kuendelea kuitumikia klabu hiyo ya Etihad.

Silva anakuwa mchezaji wa tatu kukubali kuongeza mkataba mpya na mabingwa hao wa England,akitanguliwa na Samir Nasri na Aleksandar Kolarov,na kuna taarifa kwamba wengine watakaoongeza mikataba yao na Manchester City ni pamoja na Sergio Aguero na Vincent Kompany.

Silva ana historia ya kushinda mataji mawili ya ligi kuu England, FA Cup na Capital One Cup tangu alipojiunga na City kwa dau la pauni milioni 24 akitokea klabu ya Valencia miaka minne iliyopita.

Alikuwepo pia katika kikosi cha Hispania kilichoshiriki michuano ya kombe la dunia iliyomalizika huko nchini Brazil.



No comments:

Post a Comment