Tuesday, August 12, 2014

JAVIER HERNANDEZ:NAONDOKA MANCHESTER UNITED


                                                               Javier Hernandez
                                              Kocha Luis Van Gaal

Mshambuliaji wa Manchester United, Javier Herndanez,anataka kuachana na klabu hiyo ya Old Traford na kujiunga na klabu ya mabingwa wa Italia,Juventus Turin.

Taarifa za Javier kutaka kuondoka United zimewekwa hadharani na kocha wa timu ya taifa ya Mexico,Miguel Herrera.

Mshambuliaji huyo ambaye amefunga mabao 59 katika mechi 152 katika kipindi cha misimu mine akiwa na United,mbali na Juventus kuwekwa kipaumbele cha kuhitaji huduma yake,lakini pia anawaniwa na vilabu kama Inter Milan, na mabingwa wa Hispania  Atletico Madrid pamoja na klabu ya England Southampton.




No comments:

Post a Comment