Monday, August 11, 2014

MASWALI 7 ANAYOTAKIWA KUJIBU AVEVA:KWANINI AMEMTIMUA KOCHA LOGARUSIC

                                                                                 Rais wa simba,Evans Aveva

         kikosi cha wekundu wa msimbazi simba chini ya kocha Loga

   Kocha Logarusic

Maswali yameanza kutawala kila kona ya nchi hii kufuatia kitendo cha uongozi mpya wa klabu ya simba chini ya Rais wake Evans Elieza Aveva,kumtimua kocha wao kipenzi Zdravko Logarusic (Croatia),mara tu baada ya kumalizika kwa mchezo wa kirafiki wa kusherehekea siku ya simba (simba day) ambayo hufanyika kila mwaka.


Uongozi huo mpya ulituma maskauti wake kwenda nchini Zambia kuitongoza klabu ya Zesco (wenye dhamana ya kuhakikish umeme wa uhakika unapatikana nchini Zambia) ili kuja kucheza nao mchezo huo wa kirafiki na kuwapa raha mashabiki wake katika maadhimisho ya simba day,huku wakijua fika kwamba klabu hiyo ni moto wa kuotea mbali.


Uongozi wa simba kupitia kwa makamu wake wa rais-muda mfupi tu baada ya kuingia madarakani,ukatangaza kumuongezea kandarasi ya mwaka mmoja kocha Loga,kwa madai kwamba wanaridhishwa na utendaji wake wa kazi licha ya kutoipa mafanikio waliyokuwa wakiyahitaji.


Itakumbukwa kwamba Loga awali aliingia mkataba wa muda mfupi (miezi 6) kumalizia msimu akichukua mikoba toka kwa kocha Abdalah King Kibade Mputa pamoja na msaidizi wake Jamhuri Kiwelo Julio Pereira Talantiin,wakati ambapo kikosi kikishikilia nafasi ya nne kwenye msimamo baada ya kumalizika mzunguko wa kwanza wa ligi,na tangu hapo kocha Loga akashindwa hata kwa bahati mbaya kuonesha mabadiliko na kujikuta simba inamaliza katika nafasi hiyohiyo ya nne.


Mshabiki wa simba wanajiuliza maswali:  

1.kwanini kocha Loga amefukuzwa?


2.Iweje simba ifukuze kocha kwenye bonanza?


3.Uongozi wa simba walikurupuka kumpa mkataba mpya Loga?


4.Ninini hatima ya simba katika msimu huu mpya wa ligi?


5.Kiongozi gani aaminiwe na wanasimba kuchagua kocha?


6.Kamati ya utendaji simba inajitambua?


Kama simba imefukuza kocha mchana kweupe,je mpaka ligi inamalizika itakuwa imefukuza makocha wangapi?


Haya ni baadhi tu maswali yanayoulizwa na wanachama na mashabiki wa simba,maswali ambayo bila kung’ata maneno,kupepesa macho wala kutikisa masikio-Aveva na Kaburu wanawajibu wa kujibu.

NA KUNA TETESI KWAMBA PATRICK PHIRI-NDIYE KOCHA AJAYE SIMBA

No comments:

Post a Comment