Monday, August 11, 2014

DONDOO ZA SOKA

                                                      DONDOO ZA MAGAZETI YA ULAYA:AGOSTI 11,2014


Manchester United imeongeza kitita chake nakufikia Euro milioni 50 kwaajili ya kumnunua winga wa Real Madrid,Angel di Maria, 26.
Kocha Louis van Gaal pia anahitaji9 huduma ya beki wa klabu ya Ajax Amstardam ya uholanzi, Daley Blind, 24, pamoja na kiungoi wa AC Roma, Kevin Strootman, 24.
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger yupo tayari kufufua tena mazungumzo ya kutaka kumsajili beki wa Liverpool ambaye hana uhakika na hatima yake ndani ya klabu hiyo ya Anfeld, Daniel Agger, 29.
Hata hivyo Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers, amesema bado hajapokea maombi toka klabu yeyote kuhusu usajili wa Agger.
Arsenal wanajipanga kurusha ndoano zake kuwanasa mshambuliaji wa Germany, Lukas Podolski, 29, pamoja na mshambuliaji wa Costa Rica, Joel Campbell, 22, ambao wote wanawindwa na klabu ya Uturuki- Galatasaray.
Newcastle United inaongoza mbio miongoni mwa vilabu vitatu kuiwania saini ya mchezaji kinda wa Manchester United, Wilfried Zaha, 21.
Barcelona inataka kufanya usajili madhubuti msiamu huu,na tayari imeanza kumfukuzia mshambuliaji wa zamani wa Colombia anayeitumikia klabu ya Fiorentina, Juan Cuadrado,26 – ambaye ameripotiwa kuwa United nao wanammezea mate.
Southampton wanataka kumsajili beki wa kati wa klabu ya Steaua Bucharest , Florin Gardos, 25, nab ado wanamtolea macho beki wa kushoto wa klabu ya  Sporting Lisbon ya Ureno, Marcos Rojo,24.

Everton haijathibitisha kwamba wanamuhitaji kwa mkopo winga wa Ghana,Christian Atsu, 22,kutoka Chelsea kwaajili ya msimu huu.
Kocha wa Sunderland, Gus Poyet anaiota mno huduma ya kiungo wa klabu yake ya zamani ya Brighton-Will Buckley, 24.

No comments:

Post a Comment