Thursday, August 7, 2014

BENZEMA AVITOLEA NJE VILABU VYA ENGLAND


Mshambuliaji karim Benzema,amezitolea nje ofa za vilabu vya ligi kuu ya England kwa kuamua kuongeza mkataba na klabu yake ya Real Madrid ya Hispania kwa  muda mrefu hadi mwaka 2019.

Vilabu hivyo vya England ni pamoja na wabeba mitutu wa London Arsenal, Liverpool na Tottenham,ambao wamekuwa wakipigana vikumbo kuiwania saini yake.

Benzema amefanikiwa kufunga mabao 111 katika mechi 235 tangu alipojiunga na Real Madrid mwaka 2009 akitokea kunako klabu ya Lyon.

Miongoni mwa mabao hayo 24 ameyafunga katika msimu uliopita na kuiwezesha klabu hiyo kunyakua taji la mabingwa barani ulaya.


No comments:

Post a Comment