Thursday, August 7, 2014

MADRID YACHUANA NA LIVERPOOL KUMUWANIA FALCAO.




Mshambuliaji wa klabu yaMonaco ya Ufaransa Radamel Falcao,huenda akaihama klabu yake baada ya wababe wawili kujitokeza kuhitaji huduma yake.

Falcao anahitajika sana na Real Madrid ya Hispania pamoja na vijogoo Liverpool ya England,ambao  kwa sasa wanapigana vikumbo kuona ninani anayeweza kulamba  dume kumsajili Mcolombia huyo.

Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers,yeye anahitaji kumsajili Falcao kwa mkopo wa muda mrefu,huku Madrid wakimuhitaji ili kuimarisha safu yao ya ushambuliaji.

Wakati huohuo mchezaji Loic Remy ameripotiwa kufeli katika zoezi la vipimo vya afya yake na hivyo kushindwa kujiunga na Liverpool.

Hata hivyo Liverpool pia imesitisha mpango wa kumsajili mchezaji wa Swansea City-Wilfried Bony.


No comments:

Post a Comment