Thursday, August 7, 2014

                                                   DONDOO ZA MAGAZETI YA ULAYA,AGOSTI 07/2014




Klabu ya Inter Milan ipo tayari kumruhusu kiungo wake Fredy Guarin, 28, (Mcolombia) kwenda kujiunga na mashetani wekundu- Manchester United. 
United pia ima matumaini ya kumpata mlinzi wa klabu ya Roma - Mehdi Benatia, 27 kwa kitita cha Euro 30m,lakini watalazimika kuingia katika mapambano na vilabu vya  Chelsea pamoja na  Real Madrid,ambavyo navyo vinahitaji huduma ya Benatia.

Mabingwa wa Ebgland Manchester City,itakamilisha kabisa usajili wa beki wa klabu ya FC Porto Mfaransa Eliaquim Mangala kwa dau la Euro milioni 32,mwishoni mwa wiki hii.

Wabeba mitutu wa London Arsenal wamemgeukia kiungo mshambuliaji wa klabu ya  Shakhtar Donetsk- Douglas Costa, 23,kutaka kumsajili baada ya kukwama kumsajili mchezaji wa FC Porto Juan Quintero, 21.  
Daily Express 

West Ham United inamuhitaji mshambuliaji wa Stoke City Peter Crouch, 33 – lakini wakitanguliza ofa ya Euro milioni 3 mezani. 
Telegraph 

Real Madrid wanataka kuwasajili magolikipa wa Chelsea, Petr Cech, 32, na Thibaut Courtois, 22.

Kocha wa Napoli ,Rafael Benitez,anataraji kupiga hodi kwenye klabu yake ya zamani  Liverpool kujaribu kumsajili kiungo  Lucas Leiva, 27. 

Swansea wanajiandaa kumnyakua beki wa kati wa Napoli, Federico Fernandez,25. 



No comments:

Post a Comment