Thursday, August 7, 2014

WAKALA KUAMUA ARSENAL AU LIVERPOOL KUMCHUKUA CAVAN




Wakala wa mshambuliaji wa klabu ya PSG Edison Cavan,amethibitihsa kwamba vilabu vya Arsenal na Liverpool,vimerusha ndoano ya kumuhitaji nyota huyo haraka iwezekanavyo.

Awali Cavani aliripotiwa kuihama Paris Saint-Germain msimu huu, na kutimkia kwenye ligi kuu ya England aidha kwenye klabu ya Manchester United au Chelsea,ambao walikuwa wamekaa mkao wa kula kuinasa saini yake.

Hata hivyo,kwa mujibu wa wakala huyo Claudio Anelluci,amesema vilabu vyenye nia ya dhati ya kumuhitaji Cavan ni Arsenal na Liverpool.

Wiki iliyopita Cavani alitamka wazi kwamba anajisikia furaha kuendelea kuitumikia klabu yake kwa msimu mwingine,huku  Liverpool wakimuwinda mshambuliaji wa  Monaco-Radamel Falcao.

No comments:

Post a Comment