Thursday, August 7, 2014

MAN UNITED YAIZIDI KETE BARCELONA KUHUSU VARMAELEN


Manchester United sasa imekubali kutoa Euro milioni (£15m) kwaajili ya kumsajili mlinzi wa Arsenal, Thomas Vermaelen,na kuiachia manyoya Barcelona ambao nao wanamuhitaji kwa udi na uvumba.

Kocha wa United, Louis van Gaal anataka kufanya usajili wa haraka baada ya klabu hiyo ya mashetani wekundu kurejea toka katika ziara yao ya maandalizi ya ligi huko nchini Marekani,na anataka kukamilisha usajili huo wa  Vermaelen pamoja na mcezaji wa klabu ya Ajax- Daley Blind kabla ya mchezo wao wa kwanza wa ligi dhidi ya Swansea City August 16.

Kwa upande wao Barcelona wamesema wapo tayari kuweka mezani kitita cha Euro milioni (£10m) kwaajili ya nyota huyo wa Ubeligiji.
 


No comments:

Post a Comment