Tuesday, August 5, 2014

KIUNGO WA MAN CITY-Jack Rodwell:AJIUNGA NA SUNDERLAND



Klabu ya Sunderland maarufu kama paka weusi,wamekamilisha usajili wa kiungo, Jack Rodwell toka klabu ya mabingwa wa England Manchester City.

Kiungo huyo wa England,23, amejiunga na Sunderland kwa ada ambayo haikuwekwa wazi na kuingia mkataba wa miaka mitano. 

"hii ni klabu ambayo inanifaa sana kuichezea” amesema Rodwell wakati akihojiwa na mtandao wa Sunderland.

Rodwell alijiunga na Manchester City akitokea Everton kwa ada ya pauni milioni 12 mwaka 2012,lakini ameshuka dimbani mara 26 kuitumikia klabu hiyo na kufunga magoli mawili.

No comments:

Post a Comment