Tuesday, August 5, 2014

DONDOO


                                          DONDOO ZA SOKA:MAGAZETI YA ULAYA AGOSTI 4,2014

KLABU YA Everton imeingiwa na hofu ya kumsajili winga wa Chelsea, Christian Atsu, 22,kwa mkopo kutokana na mchezaji huyo kutopewa mechi nyingi na klabu yake.

Daily Mirror 

Liverpool na Tottenham wanapigana vikumbo kutaka kujaribu kwa mara nyingine kumsajili mshambuliaji wa  Ivory Coast ,Wilfried Bony, 25, na klabu yake ya Swansea ipo tayari kumuuza kwa dau la pauni milioni £19m.
Daily Mirror 

Beki wa Ubeligiji Thomas Vermaelen, 28, hana mpango wa kufanya mazungumzo juu ya mkataba mpya na klabu yake ya Arsenal ili kuishinikiza kumfungulia milango,na tayari vilabu vya Barcelona na Manchester United,vipo tayari kumsajili kwa dau la pauni milioni  £10m.


Tottenham ipo katika hatua za mwisho za mazungumzo juu ya kumsajili kwa dau la pauni milioni £17m beki wa kati wa Argentina-Mateo Musacchio, 23,toka klabu yake ya Villarreal na Spurs ipo tayari kumfungulia mlango wa kutokea beki wake Younes Kaboul kwenda kujiunga na klabu ya Lazio ya Italia,kwa dau la pauni milioni  £6m. 


Klabu ya Sunderland ipo tayari kumsajili mshambuliaji wa zamani wa  Cameroon, Samuel Eto'o, 33,ambaye kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kutemwa na klabu yake ya Chelsea. 


Kocha wa Aston Villa, Paul Lambert anajipanga kufanya mazungumzo na mlinzi wa Uholanzi Ron Vlaar, 29,ili kumpa unahodha wa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment