Tuesday, August 5, 2014

KAGAWA,CHICHARITO BY BY UNITED

Chicharitoooooooo

                                                                  Shinjiiiiiiiii



Kocha wa Manchester United Mholanzi, Louis van Gaal, amesema mshambuliaji wake Javier Hernandez,26 (Mexico) pamoja na kiungo Shinji Kagawa,25 (Japan ),wanaweza kuuzwa kwenye klabu nyingine.


Taarifa toka ndani ya klabu hiyo ya mashetani wekundu,zinasema Van Gaal atakutana na kumueleza makamu mwenyekiti wa klabu hiyo, Ed Woodward kwamba  Hernandez na Kagawa wanaweza kuuzwa, pamoja na viungo Marouane Fellaini na Anderson,mshambuliaji Luis Nani,na hata kinda Wilfried Zaha.


Kufuatia hali hiyo tayari klabu ya Atletico Madrid wapo tayari kutoa kitita cha pauni milioni £25m ili kuzinasa saini za mshambuliaji wa Mexico Javier Hernandez, 26, na kiungo wa Ki-Japan Shinji Kagawa, 25.


Lakini hata hivyo kuna uwezekano wa Atletico Madrid kufanya mabadilishano na United kwa kumtoa Ardan Turan ili wapewe Shinji Kagawa.


No comments:

Post a Comment