Monday, August 4, 2014

GOSSIP

                Dondoo za soka:Magazeti ya ulaya,Agosti 04,2014





Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers,amepuuza taarifa za yeye kumuhitaji mshambuliaji mtukutu wa AC Milan, Mario Balotelli,baada ya kuwepo tetesi za kumuwinda nyota huyo wa timu ya taifa ya Italia.

Daily Mirror 
 
Tottenham ipo tayari kutoa kitita cha pauni milioni £17m kwaajili ya kumsajili beki wa kati wa klabu ya Villarreal na timu ya taifa ya Argentina,Mateo Musacchio,23. 

Times (subscription required) 
 
Kocha wa West Ham United, Sam Allardyce,anammezea mate mshambuliaji wa  Manchester United, Wilfried Zaha, 21,kumshusha  Upton Park. 

Mbali na mchezaji huyo,pia Spurs wanahitaji huduma ya mshambuliaji ngongoti wa  Stoke City- Peter Crouch, 33, ili kuziba pengo la Andy Carroll aliye majeruhi. 

Lakini hata hivyo mshambuliaji wa Sunderland  Connor Wickham, 21,amewekwa katika chaguo la kocha Allardyce,kuziba pengo la Carroll ambaye atakuwa nje ya dimba kwa kipindi cha miezi 4.

Daily Telegraph 
 
Meneja wa Southampton,Ronald Koeman yu tayari kumsajili kind la Manchester United mshambuliaji Demetri Mitchell,17 kwa mkopo.

 Daily Mirror 
 
Klabu ya Italia AC Milan,imeonesha nia ya dhati ya kutaka kumsajili mlinda mlango wa klabu ya Liverpool Pepe Reina,31-lakini kiwango kikubwa cha mshahara anaoutaka kipa huyo huenda kikakwamisha kabisa mpango huo.

Daily Mail  

No comments:

Post a Comment