Monday, August 4, 2014

MADRID YAMNYAKUA MLINDA MLANGO ALIYENG'ARA KOMBE LA DUNIA

                           Navas akiwa katika heka heka za kuokoa hatari langoni mwake
                         Navas akimzidi maarifa mshambuliaji wa timu pinzani na kumuachia manyoya
                       Golikipa Navas akiwapanga mabebi wake wakati akiwa na klabu ya Levante




Klabu ya Real Madrid,imekamilisha usajili wa golikipa wa Costa Rica, Keylor Navas kwa mkataba wa muda mrefu kuitumikia klabu hiyo ya Hispania.

Navas aliyeifikisha Costa Rica hadi hatua ya robo fainali kwa mara ya kwanza katika historia yake huko nchini Brazil,amekubali kuingia mkataba wa miaka 6.

Mlinda mlango huyo,27-ametua Santiago Bernabeu akitokea kunako klabu ya Levante ambayo nayo inashiriki ligi kuu ya Hispania maarufu kama La Liga.

Baada ya kukamilisha usajili huo,Madrid itamtambulisha Navas mbele ya mashabiki wake kesho jumanne mara tu baada ya kukamilisha zoezi la vipimo vya afya yake. 

Navas sasa atakuwa anagombania namba pamoja na magolikipa wenzake aliowakuta, Iker Casillas na Diego Lopez. 

Huyo anakuwa mchezaji wa tatu kujiunga na Real Madrid ambao ni mabingwa wa ulaya,baada ya kuwasajili mjerumani-Toni Kroos na MColumbia- James Rodriguez.

No comments:

Post a Comment