Monday, August 4, 2014

MASWALI MAGUMU KWA STARZ NA SOKA LA TANZANIA-TFF INAWAJIBU WA KUJIBU.



WATANZANIA bado wanaendelea kuuguza donda lisilopona katika medani ya soka,huku wakijiuliza maswali magumu yasiyojibika kila kukicha kwamba ninani anayeliroga taifa hili lisifanye vizuri katika michuano ya kimataifa?

Swali hilo hakuna mtanzania yeyote anayeweza kujibu isipokuwa wapo wachache mwenye kujaribu kutoa maelezo yenye kutafuta mwarobaini wa tatizo hilo.

Starz ilipata bahati ya kuingia katika kinyang’anyiro cha kuwania tiketi ya kucheza michuano ya kuwania kombe la mataifa ya afrika itakayofanyika mwakani kule nchini Moroco,lakini cha kushangaza imeshindwa kuonesha kama inaweza kushiriki katika michuano hiyo.

Mechi yake ya kwanza dhidi ya Zimbabwe starz ilijitahidi kufurukuta na kufanikiwa kuisukumiza nje Zimbabwe katika patashika hizo na kusonga mbele kuvaana dhidi ya Mambaz wa Msumbiji ikiwa ni hatua ya mwisho kabla ya kuvuka na kuingi akatika hatua ya makundi,lakini ikajikuta inapepesa macho katika mchezo wa kwanza uliopigwa hapa nyumbani kwa kulazimishwa sare ya mabao 2-2.

Hata hivyo matokeo hayo hayakuivunja mioyo ya watanzania wengi ambao walijipa matumaini kwamba wanaweza kupata ushindi wakiwa ugenini katika mchezo wa marudiano lakini imekuwa tofauti.

Katika uwanja wa Zimpeto huko Msumbiji,Starz imejikuta ikikubali kipigo cha mabao 2-1 na hivyo kuzima kabisa ndoto za taifa hili kucheza michuano hiyo mikubwa barani afrika.


Hapana shaka kwa hali hii jinsi ilivyo,rais wa shirikisho la kandanda la Tanzania TFF Jamal Emil Malinzi,anawajibika kubeba lawama za taifa hili kufanya vibaya katika patashika hizo kutokana na maandalizi yasiyokuwa ya kitaalamu kabla starz haijashuka dimbani.





No comments:

Post a Comment