LUIS VAN GAAL
Manchester United
bado inaonesha haijakaa sawasawa tangu ilipotoka katika wakati mgumu msimu
uliopita,kikosi hicho kikiwa chini ya kocha David Moyez aliyetimuliwa kwa aibu
ya mwaka,na kikosi hicho kukabidhiwa kwa muda mikononi mwa Ryan Giggs.
Hali hiyo ya United ya kutia shaka kwa mashabiki
wake,imeanza kujionesha leo katika patashika ya kuanza kwa ligi kuu
Engalnd,baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 mbele ya mashabiki dhidi ya
Swansea City.
Vijana hao wakiwa ugenini walikitawala kipindi cha kwanza na
kufanikiwa kupata bao katika dakika ya 28 likifungwa na mchezaji Kin Sung
Young,na kuwaacha mashabiki wa United wakiwa hoi mpaka dakika 45 za kwanza
zinamalizika.
Kipindi cha pili United wakajipapatua na kusawazisha bao
hilo katika dakika ya 53 likifungwa na mshambuliaji wao aliyetabiriwa kufanya
makubwa katika msimu huu-Wine Rooney na kuamsha angalau shangwe kwa mashabiki
wao.
Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa kocha Luis Van Gaal na vijana
wake katika dakika ya 72,pale ambapo mchezaji wa Swansea Sigardsson,alipopigilia
msumari wa mwisho kwa kuandika bao la pili na la ushindi,na kuufanya mchezo huo
kumalizika kwa United kulala nyumbani kwa mabao 2-1.
VIKOSI KAMILI KWENYE MCHEZO HUO:
UNITED: De Gea; Jones, Smalling, Blackett; Lingard (Januzaj (24min), Fletcher, Herrera (Fellaini 67), Young; Mata; Hernandez (Nani 46), Rooney. Subs: Kagawa, Michael Keane, Amos, James
SWANSEA
: Fabianski; Rangel, Amat, Williams,
Taylor (Tiendalli); Ki, Shelvey; Routledge, Sigurdsson; Dyer (Montero 67), Bony
(Gomis 77). Subs: Tiendalli, Montero, Tremmel, Bartley, Richards, Sheehan


No comments:
Post a Comment