Saturday, August 16, 2014

WENGER AANZA KWA MKWARA LIGI KUU ENGLAND,AIANGAMIZA CRYSTAL PALACE


Laurent Koscielny

Aaron Ramsey 

Kikosi cha wabeba mitutu wa London Arsenal,kimeanza vema harakati zake za kuusaka ubingwa wa ligi kuu ya England msimu huu,baada ya kuitandika mabao 2-1 Crystal Palace na kuondoka na pointi zote tatu katika mchezo uliopigwa kunako dimba la Emirates.
Kipindi cha kwanza kilikuwa ni vuta nikuvute,na katika dakika ya 35 Crystal Palace wakapata bao lililowekwa nyavuni na mchezaji Hangeland,kabla ya Arsenal hawajasawazisha bao hilo katika dakika ya 45 ikiwa ni sekunde chache tu kabla ya kipindi cha kwanza hakijamalizika,ambapo mchezaji Laurent Koscielny akaweka mambo kuwa sawa kwa sawa.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kila upande ukitaka kuibuka na ushindi,lakini upepo ukawaendea vizuri wabeba mitutu,ambapo katika dakika ya 90 mchezaji Ramsey akaamsha shangwe kwa mashabiki kwa kuandika bao la pili na la ushindi.

Ushindi huo ni ishara tosha kwa kocha Arsene Wenger ambaye amekisuka vema kikosi chake tayari kwa mapambano msimu huu.

Matokeo mengine,Leicester imekwenda sare ya kufungana mabao 2-2 dhidi ya Everton,QPR wao wamekiona cha moto baada ya kuchapwa bao 1-0 dhidi ya Hull City,Aston Villa wameishikisha adabu Stoke City kwa kuifumua bao 1-0,West Bromwich Albion nao wakienda sare ya mabao 2-2 dhidi ya Sunderland,huku West Ham wakishindwa kutamba nyumbani na kuruhusu goli moja kwa bila dhidi ya Totenham Spurs.


No comments:

Post a Comment