Wednesday, September 3, 2014

KHEDIRA,BOATENG,HUMMELS,NJE UJERUMANI IKICHEZA NA ARGENTINA LEO

                                   Kocha Joachim Low,akikuna kichwa kuiwazia Argentina


KIUNGO wa Real Madrid,Sami Khedira,atakuwa nje ya kikosi cha taifa lake la Ujerumani kitakachocheza dhidi ya Argentina na baadaye Scotland,kutokana na kupata majeraha.

Shirikisho la kandanda nchini Ujerumani,limethibitisha jana kwamba mchezaji huyo atakuwa nje ya uwanja kutokana na matatizo hayo.

Kocha mkuu wa Ujerumani,Joachim Loew,tayari amemuita kiungo wa klabu ya Hoffenheim  Sebastian Rudy ,ambaye atashuka dimbani na kikosi hicho usiku wa leo kuziba pengo hilo la kiungo mkabaji.

Rudy, 24, alikuwemo katika kikosi cha Ujerumani kilichotoka sare ya bila kufunga dhidi ya Poland katika mchezo wa kirafiki uliopigwa mei 13 kabla ya kuanza patashika ya michuano ya kombe la dunia.

Naye mlinzi ,Jerome Boateng wa Bayern Munich pamoja na Mats Hummels wa Dortmund,pia hawatakuwemo kwenye kikosi cha kocha Low,kutokana na kupata majeraha jana wakiwa katika mazoezi,lakini kiungo wa Arsenal, Mesut Ozil,naye akienguliwa mapema kwenye kikosi hicho kutokana na kuumia kifundo cha mguu.

Lakini hata hivyo,nahodha mpya wa Ujerumani,Bastian Schweinsteiger naye ameripotiwa kusumbuliwa na goti, huku Philipp Lahm, Miroslav Klose na Per Mertesacker,wakiwa tayari wamestaafu kuitumikia timu hiyo ya taifa,nah ii inamaanisha kuwa Ujerumani huenda ikakwaa kisiki mbele ya Argentina,ambayo ilifungwa katika mchezo wa fainali ya kombe la dunia huko brazil.


No comments:

Post a Comment