Thursday, September 4, 2014

LAHM,KLOSE,MERTESACKER-WAPEWA TUZO ZA HESHIMA BAADA YA KUSTAAFU TIMU YA TAIFA

                                 Tuzo za heshima zina raha yake

WAKONGWE Miroslav Klose, Philipp Lahm na Per Mertesacker wamepewa tuzo za heshima usiku huu kabla ya mchezo wa kirafiki kati ya Ujerumani na Argentina Uwanja wa Esprit Arena.
Watatu hao waliichezea Ujerumani katika fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2014 dhidi ya Argentina kabla ya kuamua kustaafu soka ya kimataifa.
Klose, ambaye ni mfungaji bora wa kihistoria wa Ujerumani kwa mabao yake 71, ametungika daluga baada ya kuwa mfungaji wa mabao mengi zaidi katika historia ya Kombe la Dunia.
MCHANGO WAO KATIKA TIMU YA TAIFA UJERUMANI...
Miroslav Klose (Lazio) - Mechi 137, mabao 71 
Philipp Lahm (Bayern Munich) - Mechi 113, mabao 5
Per Mertesacker (Arsenal) - Mechi 104, mabao 4


No comments:

Post a Comment